Usafishaji wa fukwe Kidimbwi beach ( Beach cleanup)

Green Awareness Club Yashiriki Zoezi la Usafi Kidimbwi Beach – Kinondoni

27 Agosti 2022 | Kidimbwi Beach, Bahari ya Hindi | Kinondoni


Ushirikiano wa Kulinda Mazingira ya Bahari

Mnamo tarehe 27.08.2022, Green Awareness Club ilishiriki zoezi la kufanya usafi katika eneo la Kidimbwi Beach, Bahari ya Hindi, kwa kushirikiana na Environmental Conservation Community of Tanzania (ECCT). Mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Godwin Gongwe, ambaye ameendelea kuhamasisha jamii kushiriki zoezi la usafi kila mwisho wa mwezi.

Mhe Godwin Gongwe akishiriki zoezi la usafi Kidimbwi Beach Kinondoni
Mheshimiwa Godwin Gongwe akishiriki zoezi la usafi.

Wananchi Wajitokeza kwa Wingi

Wananchi mbalimbali, vijana na wanachama wa Green Awareness Club walijitokeza kushiriki katika ukusanyaji wa taka, hususan plastiki zinazochafua mazingira ya pwani. Zoezi hili limeonesha mshikamano wa jamii katika kulinda mazingira ya Bahari ya Hindi.

Wanachama wa Green Awareness Club wakifanya usafi Kidimbwi Beach Zoezi la usafi wa fukwe Kinondoni Wananchi mbalimbali waliojitokeza kushiriki usafi Zoezi la usafi Kidimbwi Beach 2022 Wananchi wakikusanya taka pwani ya Bahari ya Hindi Green Awareness Club Kidimbwi Beach clean up
Mhe Godwin Gongwe na Ibrahim Sinsakala Kidimbwi Beach
Kutoka Kushoto: Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Godwin Gongwe na Mwenyekiti wa Green Awareness Club Ndugu Ibrahim Sinsakala.

🌿 Mazingira safi, Mazingira ya kijani🌿